Русские видео

Сейчас в тренде

Иностранные видео


Скачать с ютуб ADINANI HUSSEIN ANATAFUTWA KWA TUHUMA ZA UTEKAJI WA WAFANYABIASHARA - KAMANDA MULIRO AELEZA... в хорошем качестве

ADINANI HUSSEIN ANATAFUTWA KWA TUHUMA ZA UTEKAJI WA WAFANYABIASHARA - KAMANDA MULIRO AELEZA... 4 недели назад


Если кнопки скачивания не загрузились НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу страницы.
Спасибо за использование сервиса savevideohd.ru



ADINANI HUSSEIN ANATAFUTWA KWA TUHUMA ZA UTEKAJI WA WAFANYABIASHARA - KAMANDA MULIRO AELEZA...

ADINANI HUSSEIN ANATAFUTWA KWA TUHUMA ZA UTEKAJI WA WAFANYABIASHARA - KAMANDA MULIRO AELEZA... Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam SACP Muliro J. Muliro amesema Jeshi la Polisi linaendelea kuchunguza na linafuatilia kwa karibu taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na taarifa ya  kupotea kwa mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Adinani Hussein Mbezi @adam (32) mkazi wa Kinyerezi. Kwa mujibu wa taarifa hiyo inadai kuwa mtu huyu alikamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza na kusafirishwa hadi Dar es Salaam ambapo inadaiwa alikuwa akihamishwa katika vituo mbalimbali vya Polisi Dar es salaam, huku ndugu wakipigiwa simu na wanaodaiwa kuwa ni askari Polisi kwa namba tofauti tofauti na  kuombwa watume pesa kupitia namba za simu mbalimbali ili ndugu yao aweze kuachiwa huru ambapo mpaka sasa hawajamuona ndugu yao na baadae simu hizo zikawa hazipatikani. Ukweli wa tukio hili ni kwamba, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamtafuta mtu huyo anayejulikana kwa jina la Adinani Hussein Mbezi @adam na wenzake kwa tuhuma za kuteka watu hasa wafanyabisahara wakubwa huku wakati wakitenda makosa hayo walikuwa wakijitambulisha kama maafisa wa TAKUKURU, TRA, Polisi au Usamala wa Taifa. Watuhumiwa hao tarehe 11 Septemba 2023 walimteka mtu mmoja mwenye asili ya Kihindi aliyejulikana kwa jina la Maaz Mohamed (27) mkazi wa Upanga  saa 5:05 asubuhi  maeneo ya barabara ya Bibi Titi wakamnyang’anya shs 357,000,000 na USD 38,000  walimuachia baada ya kupora pesa hizo kwa sharti la baadae kuwamalizia kiasi cha pesa shs 100,000,000 vinginevyo watapoteza maisha yake. Baada ya Polisi kupata taarifa tarehe 12 Septemba 2023 saa 8 mchana  waliwekewa mtego maeneo ya Daraja la Tanzanite walipotaka kumteka tena mfanyabiashara huyo huyo na  walipotaka kukamatwa walikurupuka na gari lenye namba T 146 DPY  ambalo baadae walilitelekeza eneo la Muhimbili wakakimbia. Gari lilivutwa na Polisi na kuwekwa kituo cha Polisi Salenda bridge kama sehemu ya kielelezo cha tukio hilo la kumteka mfanyabiashara huyo. Watuhumiwa hao bado wanatafutwa na si kweli kwamba walikamatwa Mwanza na kuletwa Dar es Salaam na kuzungushwa kwenye vituo vinavyotajwa, na taarifa hiyo iliyotolewa sio ya kweli. Namba hizo za simu zilizotajwa yaelekea zilitumiwa na matapeli wakawatapeli pesa wahusika na ndio maana baada ya utapeli hawakupatikana tena Jishindie Zawadi na Global TV Jaza sehemu zifuatazo hapo chini ili kuingia kwenye droo ya kujishindia zawadi mbali mbali na Global TV 👉🔥👉https://forms.gle/aU9zsYyXNyKWmd3f7 ============================================================ ⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI? ⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 713 750910), ( +255 783453136) ⚫️ Email: [email protected] ⚫️ OUR PLAYLISTS: ⚫️ MICHEZO na BURUDANI:    • Habari zote za michezo na Burudani Ta...   ⚫️ HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: http://bit.ly/mikasa_ya_kusisimua ⚫️ GLOBAL RADIO TV: http://bit.ly/255globalradio ⚫️ EXCLUSIVE INTERVIEW: http://bit.ly/exclusive_interviews ⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: http://ndstream.net/globalradio/ ⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Comments